Tiba asili ni huduma za kiafya za kiasili zinazopatikana na kwa kila jamii kwa madhumuni ya kutambua, kukinga kutibu na kuboresha mwili kutokana na magonjwa pamoja na maradhi mbalimbali.
TIBA ASILI NI NINI?
Tiba asili ni huduma za kiafya za kiasili zinazopatikana na kwa kila jamii kwa madhumuni ya kutambua, kukinga kutibu na kuboresha mwili kutokana na magonjwa pamoja na maradhi mbalimbali. Huduma hizi zitolewazo na watu wa aina mbalimbali kwa kutumia nyenzo, ujuzi na uzoefu wa kiasili. Tiba asilia hutofautiana toka jamii au kabila moja hadi jingine. Baadhi ya dawa au tiba toka jamii zingine zina ubora wa kipekee kiasi cha kuleta mvuto sehemu zingine.
MGANGA MAANA YAKE NINI
Kwa kawaida mganga wa tiba asili ni mtu yeyote mwenye elimu na uzoefu wa taaluma ya tiba asili ambaye anakubalika na kutambulika na jamii anamoishi, uzoefu wake wa kutoa huduma unatokana na kusomea na kurithi au kufanya kazi na mtaalamu kwenye uzoefu wa taaluma hiyo.
KAZI ZA MGANGA WA TIBA ZA ASILI
Mganga wa tiba asili aliyopata mafunzo anatarajiwa kufanya yafuatayo:-
SISITIZO
MAUAJI YA KIKATIRI
Mauaji ya kikatiri – Maana yake ni kwamba watu wanachinjwa kama wanyama / kuku mfano mauaji ambayo yanayotokea mkoa wa Mara ni yakinyama, hasa wilaya ya Butiama yote imeshakuwa ya rahana kubwa. Baada ya kufanya utafiti wa kina zaidi Shimautita tuligundua kuwa watu hao wengi wao si wachawi, ni fitina za mtu na mtu anaenda kukodisha watu wakuja kwa kutumia mapanga, wengine ni fitina za mashamba, wengine ni wategaji wa samaki, mfano wavuvi wa dagaa na sangara wanaua watu sana, pamoja na machimbo kwa uchunguzi zaidi, na wengine watu wanaowaendea waganga ili kupiga ramri – za ndagu za kuua ili kupata utajiri wa haraka.
SISITIZO waganga acheni kupiga ramri kama hizo hazina maana, pia ni kudhalilisha nchi na kufanya tiba asili ikoswe thamani. Ebu angalia nchi kama China ilivyoendelea kwa madawa ya asili, tusirudishe tiba yetu ya asilia kama vile wageni walivyoingia na kuikandamiza ili ikose uthamani wake, mfano nchi ya Kijerumani na Uingereza zilikuwa hazitaki kabisa mwafrika atowe hii huduma ya tiba asili.
Ukizingatia tiba asili ilikubalika na serikali yetu toka mwaka 1974 ndipo ilianza kutambulika.
Baada ya Uhuru, tiba asilia zilikuwa chini ya Wizara ya Utamaduni mpaka mwaka 1989, tarehe 4th mwezi Oct mwaka 1989. Katika kikao kilichofanyika Dodoma mjini, ndipo kitengo hiki Kiliamishiwa Wizara ya afya - na toka kiamie Wizara ya afya kina miaka 24 lakini kikawa kimeifadhiwa ofisini tu, bila mwendelezo wowote. Mpaka kufika mwaka 2001 ndipo wakaanza kutunga sera ya tiba asilia na kupitishwa kwa sera hii ya tiba asili na tiba mbadala. Bungeni na sheria ya tiba asili na kupitishwa 2002.
Sheria 23/2002 na kuzinduliwa kwa tiba ya mwafrika mwaka 2005, lakini sheria hiyo? Sheria hiyo haieleweki kwamba mpaka sasa inaranya kaiz gani?, Ombi sheria iwafikie walengwa na mabaraza yaundwe huko mikoani ili waganga waweze kutambua wajibu wa kazi zao.
USAFI NA MAZINGIRA
Wagonjwa walazwe mahala pasafi, vyombo vya kuifadhia madawa na mahala pa kutunzia madawa pawe pasafi, wembe uwe safi.
Pia anapo fanyia kazi pawe safi, vyoo viwili vyote viwe safi mabafu yote mawili yawe safi, hadi marazi ya mganga mwenyewe yawe safi.
MADHARA YA UCHAFU
Unapokuwa unatoa huduma ukiwa mchafu basi unaweza kumuongezea mgonjwa wako magonjwa mengine, kumsababishia kuharisha, pumu, vikoozi vya kila wakati, ukimwi, pepopunda, funza, upele, ukurutu, kichocho na kunywa dawa zako bila imani anaweza kuondoka bila kupona.
KUJIKINGA NA UCHAFU ILI USIPATE MARADHI YA KUAMBUKIZWA NA MTEJA
Ukibainika lazima shirika hili litakushitaki na mwananchi yeyote Yule atakaye enda kwa mganga akafanyiwa tendo hilo uende moja kwa moja kwa daktari athibitishe kisheria tuletee hiyo barua, lazima ashitakiwe na kusimamishwa kazi yake kwa kushirikiana na serikali husika.
MGANGA TAPELI
Wapo watu wasiokuwa na taaluma ya tiba asili au wanautambuzi mdogo sana kwa taaluma hii.
Wapo wasioijua hii taaluma kazi yao ni kununua dawa kutoka kwa wataaluma, baadaye kujifanya kuwa wenyewe ndiyo wataaluma zaidi.
Hizo ni dalili za kumtambua mtapeli na wao wanajipenda sana zaidi ya mganga mwenyewe na gharama zao ni kubwa zaidi.
MAADILI YA TIBA ASILI
Mganga wa jadi /wana taaluma wanahitaji kuzingatia maadili ya dawa, kazi zao.
MUNGU ALISHA TUPA UTAJILI WA KUTOSHA ALITUPENDELEA SISI WATANZANIA.
Mizizi yote ni dawa, magome, ni dawa, majani ni dawa na chakula na mti wake ni dawa.
Vyote ni dawa ngozi, mifupa, nyama yake vyote ni dawa.
FAIDA YA DAWA ZA ASILI
Ndugu wananchi tunaomba tuzingatie utamaduni wetu na mila na desturi usomi, dini na siasa vimepotosha mila yetu na kubakia kuthamini mila za kigeni Wananchi tugeuze akili zetu tutumie zaidi dawa zetu za asili ili tuweze kupunguza vifo vingi hapa nchini. Pia tule vyakula vya asili, mfano vyakula vyote vya nafaka na mafuta ya asili, mtaona mabadiliko ya nchi yenu kuwa makubwa kwa afya za binadam hata vifo vitapungua hapa nchini.
Mnaona magonjwa yanazidi kila kunapokucha na tiba hazipo zimebakia za wasiwasi. Nimatumaini kuwa wananchi watabadili fikira zao ili waokowe maisha yao.
Pia shirika hili ni kwa kila mtu, ili mradi anapenda shughuli za maendeleo na pia ina sekta mbalimbali ndani ya katiba ya Shimautita.
SEKTA ZILIZOMO NDANI YA SHIRIKA HILI / VITENGO