Maradhi ya pumu (Asthma)

Maradhi ya pumu huzuka kwa sababu ya kunywea mishipa iliyozunguka sehemu za mapafu.pia huwa ni kwa sababu ya maumbile yasiyo ya kawaida katika kifua ambayo mtoto huzaliwa nayo .Na katika hali hii maradhi huanza mapema katika maisha ya mtu.

Magonjwa ya pumu

Pumu huanza kwa kuvuta pumzi haraka haraka na kwa sauti ya kusikia.Mgonjwa wa maradhi haya anaweza kujisikia kubanwa pumzi na kutwetwa nyakati za asubuhi ,hali ambayo humfanya ang’ang’ane ili aweze kuvuta hewa . Baada ya juhudi hiyo,kufuatia kikohozi na kisha kutoa balaghamu kavu. hapo mgonjwa atajisikia nafuu kidogo.Halafu kikohozi na balagham kuendelea mpaka atakapopona.

Kuna sababu nyingi zinazosababisha mbano wa pumu,kama vile hali ya hewa kuwa baridi na kula baadhi ya vyakula kama nyama na samaki, au baada ya kula chakua kizito masaa ya jioni.Hivyo basi ,  kwanza  mgonjwa ajue sababu ya pumu, na ajiepushe navyo vitu hivyo vinaweza kuwa maji baridi,vumbi na vinginevyo. Mgonjwa wa pumu ni lazima nyumba yake iwe na madirisha makumbwa ya kutosha.

TIBA

  1. Pumu hutibiwa kwa kunywa dawa ya RT pamoja na MZ vipindi vilivyo sawa kiasi cha kijiko kidogo kila baada ya kula .yaani mara tatu kwa siku.
  2.  Mchanganyiko wa dawa za MCNC na ASB atakunywa kwenye kikombe cha chai kutwa mara tatu muda wa mwezi mmoja.


 


© 2025 Shirika la Maendeleo Utafiti na Tiba Tanzania - SHIMAUTITA